UJASILIAMALI MDOGO NACHINGWEA.
KIKUNDI CHA
WANAWAKE WAJANE NA WANAWAKE WAISHIO KATIKA MAZINGIRA HATARISHI
UTANGULIZI
Katika kuguswa na jamii pamoja na maisha ya kila siku ya
wanawake wajane ndio kulikopelekea kikundi cha NISHIKE MKONO kuanzishwa kikiwa
na lengo kuu la kuwafanya wanawake wajane wajikwamue kiuchumi na kuwafanya
wasiteteleke hasa baada ya kuondokewa na wenzi wao ambao kwa kiasi kikubwa ndio
walikuwa tegemeo katika maisha yao ya kila siku. Hii ni kutokana na wanawake
wengi kuwa mama wa nyumbani wakati waume zao wakiwa ndio nguzo ya familia kwa
mahitaji yote muhimu kama vile kusomesha watoto, chakula na mambo yote ya
kifamilia.
NAMBA
|
JINA LA MWANACHAMA
|
CHEO
|
1
|
HAMISI KAMBONA
|
MWENYEKITI/MWEZESHAJI
UJASILIA MALI
|
2
|
MWAJUMA ALLY DADY
|
KATIBU
|
3
|
ANIFA MPILI
|
MWEKA HAZINA
|
4
|
ZAINABU ABASI
|
MWANACHAMA
|
5
|
ELIZABERTH STAMBULI
|
MWANACHAMA
|
6
|
MARISELA JACKSON PETER
|
MWANACHAMA
|
7
|
STELA KIMBUNGA
|
MWANACHAMA
|
8
|
SAKINA MAPUNDA
|
MWANACHAMA
|
9
|
SHAKILA LIBABA
|
MWANACHAMA
|
10
|
BINADA MAKWALILO
|
MWANACHAMA
|
11
|
SCOLASTICA MJUMBA
|
MWANACHAMA
|
12
|
CHAUSIKU MSHANGANI
|
MWANACHAMA
|
13
|
MARIAMU CHINGUILE
|
MWANACHAMA
|
Kikundi kilianzishwa mwaka mwezi julai 2018 kikiwa na jumla
ya wanachama 13 ambao wamegawanyika katika makundi mawili ambayo ni kundi la uongozi na ushauri na kundi la
wanachama wajane. Kama yaliyoainishwa hapa chini katika jedwali lifuatalo;
MALENGO YA KIKUNDI
Malengo ya kikundi cha NISHIKE
MKONO MJANE yamegawanyika katika makundi matatu yote yakiwa na umuhimu
unaolenga kumuinua mjane ili aishi kama mwanzo na kumuondolea upweke na mawazo
na kumfanya shupavu na mwenye nguvu. Malengo haya ni kama yafuatayo hapa chini.
1. Kuinuana kiuchumi.
Kuinuana kiuchumi ni moja kati ya
malengo ya kikundi chetu, ambapo wakati tunaanzisha kikundi chetu ni baada ya
kuvunja kikundi cha vikoba ambapo akina mama walipata pesa ndogo sana ambayo
isingeweza kuwasaidia kwa lolote kwasababu pesa waliyokuwa wakichangia ni ndogo
sana. Hapo ndipo lilipopatikana wazo a kuunda kikundi cha wajane cha kusaidiana.
Kama wamama wajane tulichanga pesa
kidogo na kuanziasha biashara ndogo ya kupika maandazi kwa kuwekeana zamu na
pesa kuzitunza kidogokidogo. Pesa ilipoongezeka kiasi tulianza kukopeshana
wenyewe kwa mtu aliyekuwa na wazo la biashara.
2. Kupeana elimu na uzoefu katika ujasilia
mali.
Kikundi kina lengo la kupeana
uzoefu na elimu ya ujasilia mali. Kikundi kimedhamilia kutoa elimu ya jinsi ya
kuthubutu na kuzitumia fursa zilizopo katika kujikwamua kiuchumi. Tumekuwa
tukipata elimu ya ujasilia mali kwa wajasiliamali wenzetu na kupeana uzoefu
mbalimbali ambao umetujengea uwezo na
kuwa majasili wa kuzitumia fursa.
3. Kufarijiana na kushauriana katika
maisha.
Lengo la tatu la kikundi chetu ni
kufarijiana na kupeana matumaini hasa pale mtu anapokosa matumaini na kukata
tamaa kabisa. Wapo wenzetu waliobobea katika kutoa elimu ya ushauri nasaa na
kufarijiana hasa wakati wa shida kama vile ugonjwa, mawazo, madeni na n.k.
MAFANIKIO YA
KIKUNDI
Kikundi kimepata mafanikio kiasi pamoja na changamoto nyingi
tunazozipitia kila siku katika kukiendeleza kikundi chetu. Pamoja na mazuri
tuliyoyafanya na kupata, yafuatayo tunajivunia
1.
Tumeanzisha mradi wa kufuga kuku wa kienyeji
katika banda letu dogo tuliloliazima kutoka kwa mwanakikundi mwenzetu. Una
jumla ya kuku 50 wakiwemo makoo 40 na majogoo 10 ambao tumeanza nao kwa
kuwanunua kwa jumla ya shs 500000 kwa bei @ 10000/=. Wameanza kutaga mayai
tayari. Pia tuna bata 10 ambao kila mwanakikundi alileta kutokana na mkakati
wetu tuliojiwekea na katiba ya kikundi chetu.
2.
Tumefanikiwa kununua kiwanja ambacho nia na
malengo yetu tujenge ofisi zetu za ujasilia mali za kikundi ili kurahisisha
mikutano na shughuli zetu kukwepa hali ya sasa ya kukutana nyumbani kwa mtu.
Hii itasaidia kukikuza kikundi chetu na kufanya watu na jamii inufaike na kile
tunachokifanya. Kiwanja chetu kina ukubwa wa square mita 450 ambacho kitatosha
kwa kazi zetu kwa sasa.
3.
Tuna ratiba ya kukutana kila siku ya jumapili
ili kukaa pamoja na kujadiliana na kupeana ushauri wa baadhi ya mambo na
changamoto, achilia mbali siku za kukutana za kawaida za kikundi ambazo ni
jumatano na jumamosi kwa jumla pamoja na kila siku kwa wale wenye ratiba katika
kikundi chetu hasa zile za kuwahudumia kuku.
4.
Tunatoa mikopo isiyo na riba kwa wamama wajane
ambao ndo walengwa, pia tunatoa mikopo kwa wamama wengine ambao sio wanachama
kwa riba ya 5% ili kuhamasisha akina mama wajiunge katika kikundi chetu ili
wanufaike na kikundi hiki pamoja na kuongeza mtaji wa kikundi chetu.
CHANGAMOTO
Kama kikundi tuna changamoto nyingi zinazotukabili ambazo
zinatufanya kasi yetu katika kikiendeleza kikundi kupungua na kutaka kupunguza
nguvu kwa wanachama. Zipo tulizokabiliana nazo na zile zinazotushinda kuzitatua
kutokana na uwezo mdogo wa kiuchumi wa kikundi chetu. Changamoto hizi tumezigawa
katika makundi matatu kama zinavyofafanuliwa hapa chini
(a) Mtaji mdogo
Tuna mtaji mdogo wa kuendesha kikundi kiasi
ambacho kuna wakati mwanakikundi anaweza kuhitaji mkopo na asipate kwa wakati
mpaka muda wa marejesho kwa mwanachama mwingine aliyeazima pesa anaporudisha
ndio unakuwa wasaa wa mtu mwingine kuchukua mkopo, tena kwa kiwango kisichokidhi
mahitaji yake ya mkopo kwa wakati huo, hali inayofanya malengo ya wanachama
yasitimie katika ujasiliamali wetu.
(b) Mapokeo ya jamii
Kwakuwa kikundi hiki ndio kinaanza,
tunakutana na changamoto ya kutopokelewa vizuri katika jamii kutokana na wingi
wa vikundi vingi vilivyoanzishwa visivyokuwa na tija wala malengo sahii ndani
ya jamii. Tunakabiliana nazo changamoto hizi kwa kufanya kazi kwa bidii ili waaminishwe
na mafanikio yetu hapo baadae kama malengo na matarajio yetu yalivyo na ukomavu
wetu wa kupambana na changamoto nadani ya kikundi chetu. Tunaamini siku moja
jamii itatuelewa nini tunafanya na nini hasa malengo ya kikundi chetu.
(c) Mfumo dume
Changamoto nyingine ni mfumo dume ambao
unapelekea wababa wengi kuona aibu kuja kukopa kwenye kikundi chetu wakiamini
kama hatuwezi kuwakopesha japo kidogo na kutudharau hasa pale tunavyotoa elimu
ndogo kwa wajasiliamali ambao wameanza kuona mafanikio yetu na kuwa na mitazamo
ya mbali yenye mafanikio.
MAHITAJI YA
KIKUNDI
Kama kikundi tunaomba msaada wa kiasi cha pesa cha Tshs
10047500/= sawa na dollor 4067.814 za
kimarekani ili kukiendeleza kikundi chetu kichanga kama mchanganuo wa matumizi
yafuatayo kwenye jeduali hapa chini.
AINA YA MATUMIZI
|
MCHANGANUO
|
KIASI (TSHS)
|
KIASI (USD)
|
KUONGEZA MRADI WA KUKU
|
1120000
|
453.4413
|
|
KUNUNUA MADAWA NA CHANJO
|
6KG @ 30000
|
180000
|
72.87449
|
VYOMBO VYA CHAKULA NA MAJI
|
20 PC@15000
|
300000
|
121.4575
|
POSHO YA MTAALAMU WA UJASILIAMALI
|
SIKU 4/MWEZI @ 15000
|
720000
|
291.498
|
POSHO YA MLINZI WA BANDA
|
1 @ 50000/MIEZI 12
|
600000
|
242.915
|
GHARAMA ZA UENDESHAJI WA KIKUNDI
|
MATUMIZI MADOGO
|
100000
|
40.48583
|
MIKOPO KWA WAMAMA
|
25 @ 200000
|
5000000
|
2024.291
|
BIMA ZA AFYA YA JAMII (CHF)
|
20 @ 15000
|
300000
|
121.4575
|
VITAMBULISHO VYA WAJASILIA MALI
|
20 @ 20000
|
400000
|
161.9433
|
VITABU VYA KUMBUKUMBU
|
90000
|
36.43725
|
|
VIFAA VINGINE
|
10000
|
10000
|
4.048583
|
UKARABATI WA BANDA
|
|||
1. KUWEKA TAA KUBWA
|
5 @5000
|
25000
|
10.12146
|
2. GHARAMA ZA WAYA
|
MITA 15 @ 3500
|
52500
|
21.25506
|
3. FUNDI UMEME
|
1 @ 150000
|
150000
|
60.72874
|
AKIBA YA KIKUNDI
|
DHARULA
|
100000
|
404.8583
|
JUMLA KUU
|
10047500
|
4067.814
|
UWAJIBIKAJI NA
KUKIKUZA KIKUNDI CHETU
Kama kikundi tumejizatiti kuwa mfano wa kuigwa katika jamii
yetu, hivyo tunatarajia kufanya mambo makubwa ambayo yatakuwa mfano wa kuigwa
katika jamii yetu inayotuzunguka na ikiwezekana hata Taifa kwa ujumla.
Tunaamini tutakuwa mfano wa kuigwa na kioo bora kwa jamii kitakachowavutia
wajane wengi kujiunga na sisi na kuwakwamua kiuchumi zaidi.
HITIMISHO
Tunatanguliza shukurani zetu za dhati,
HAMISI KAMBONA
MWENYEKITI KIKUNDI CHA WAJANE CHA NISHIKE MKONO
NACHINGWEA-LINDI.
0714427055
Comments
Post a Comment